Monday 17 March 2014

VITAMBULISHO TANZANIA NA HOJA YA UGHAIBUNI...

Baadhi ya wananchi karibuni wamelalamikia suala jipya la vitambulisho. Wanadai linakera; eti  watu wameuawa. Kuna upendeleo. Ugumu, nk.
Kabla ya kusafiri ughaibuni miaka thelathini iliyopita  wakati wanamgambo walipokuwa wakisimamisha simamisha wazalendo mimi vile vile  nililiona suala la vitambulisho  ni unyanyasaji wa serikali. Ila baada ya kutembea na kuishi nchi nyingi duniani nimegundua  vitambulisho ni jambo la kawaida. Tofauti ipo namna vinavyoulizwa au vipi sera hii inavyotekelezwa na vyombo husika.
Tunavyojua suala la vitambulisho liliasisiwa Tanzania mwaka 1968 kwa sababu za kiusalama baina ya nchi jirani marafiki- Afrika Mashariki na Kati. Baada ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuvunjika (kutokana na sababu mbalimbali mojawapo kufariki Rais Jomo Kenyatta wa Kenya, 1978 na serikali dhalili ya Jemadari Idi Amin wa Uganda iliyoangushwa 1979), sera ilifyata. Hadi leo suala hili  limekuwa likifufuka fufuka na kutoweka, bila kujikita na kukaa kitako muda mrefu kama ilivyo mataifa mengine. Ndiyo maana leo  ni jambo geni na kero kwa raia, hasa vijana.
Idi Amin na Jomo Kenyatta -  miaka ya Sabini. Picha ya Kwekudee Blog

Mamlaka ya vitambulisho Tanzania(NIDA)- imeorodhesha vipengele kumi na moja vinavyoelezea faida zake kuu. Ndani ya orodha –  kipengele cha saba kinaahidi vitambulisho “vitafanikisha kuhakikisha kuwa mtu anapata stahili zake za jamii. Kwa mfano, kupata malipo ya pensheni, haki za pensheni, haki za matibabu, haki za kujiunga na masomo ikiwa ni pamoja na stahili zozote ambazo raia Tanzania anastahili.”
Kimtazamo ni ahadi nzuri na muhimu. Naomba nichangie namna mambo yanavyokuwa huku Ughaibuni. 



Thursday 6 March 2014

TANZANIAN PUBLISHES BOOK ON RUSSIAN EXPERIENCES DURING SOCIALIST ERA...


Some books have to be written. They must be published not for ego, money and fame - but future generations.
 “An African Student in Russia- Soviet Union” by Dr Onesphor Kyara is that type. Having failed to find a publisher (one of rejection slips hurled back by the mighty Penguin) Dr Kyara decided to self-publish. Thanks to our golden era of internet and information technology self publishing is easy in 2014.
 Available on Amazon,  E-bay, Apple i- books, as well Burns and Noble /Nook, “An African Student in Russia-Soviet Union” will soon reach  Africa based readers if Dr Kyara’s efforts succeed through  Mkuki na Nyota, local bookshops and South Africa’s Kalahari.
These are  early days.
It has only been two months...
 At the height of Ujamaa policies and the international cold war it was taboo to say certain things. 

Kyara and Marina at the height of their romance and subsequent marriage. The interesting book tells it all...